Saturday, October 26, 2013

KANUNI BORA ZA USALAMA WA KOMPYUTA YAKO

via MWANANCHI COMMUNICATION LTD


Kijana akitumia Kompyuta. Utandawazi unailazimisha dunia kuendesha mambo kwa njia za sayansi na teknolojia ikiwa ni pamoja na matumizi ya kompyuta na vifaa vingine vya kisasa.
Na Mkata Nyoni
, Mwananchi Communication LTD



Kwa ufupi

Cha msingi ni kufuata tu kanuni, kwani kwa kufanya hivyo unaweza kwa kiasi kikubwa kuepukana na mambo mengi yanayoweza kuhatarisha usalama wa kompyuta yako kama vile athari za virusi.


Ingawa mara nyingi husemwa kuwa hakuna usalama wa asilimia mia moja kwenye ulimwengu wa teknolojia ya kompyuta, ila kinga ni bora kuliko tiba.

Umewahi kujiuliza kwa nini watu wengi wanatumia kiasi kikubwa cha fedha kuimarisha ulinzi katika maeneo yao ya makazi?

Ndivyo ilivyo, tembelea hata katika makazi ya watu wa kawaida, madirisha yamejaa nondo, nyumba zimezungukwa na kuta ndefundefu. Wengine wamefikia hatua ya kufuga mbwa kwa ajili ya kuwalinda.

Nimeanza kwa kutoa mifano hii kuonyesha umuhimu wa kuzilinda kompyuta zetu. Ingawa mara nyingi husikika ikisemwa kuwa hakuna usalama wa asilimia mia moja kwenye ulimwengu wa teknolojia ya kompyuta, ila kinga ni bora kuliko tiba.

Cha msingi ni kufuata tu kanuni, kwani kwa kufanya hivyo unaweza kwa kiasi kikubwa kuepukana na mambo mengi yanayoweza kuhatarisha usalama wa kompyuta yako kama vile athari za virusi.

Makala haya yanataja baadhi ya kanuni za msingi unazopaswa kufuata ili kutunza usalama wa kompyuta yako.

Tumia programu unazozihitaji


Watumiaji wengi wa kompyuta tumekuwa waathirika wa matatizo ya kompyuta zetu ama kwa kujua au kwa kutokujua. Kwanza ieleweke kuwa kompyuta nyingi zimekuwa zikiathiriwa kiusalama kwa makosa yaliyomo kwenye kompyuta husika.

Hizi ni zile kompyuta zenye programu ambazo hazijaandikwa kiusahihi. Tuchukue mfano wa nyumba inayovuja, kwa kuwa tu paa lake halikuezekwa ipasavyo. Au ukuta wa nyumba unavyoweza kuanguka, kwa kuwa haukutengenezwa kwa kufuata taratibu za ujenzi.

Kama kompyuta yako ina programu ambayo haikuandikwa kwa usahihi, matatizo mengi hutokea yanayoweza kuhatarisha kifaa hicho. Programu hizi sio tu zitahitilafiana na mtambo endeshi (OS) wa kompyuta yako, pia zinaweza kutoa mianya kwa wavamizi kuingia kwenye kompyuta yako kupitia kwenye mianya iliyopo kwenye programu hizi.

Cha kufanya: Mosi, ondoa programu usizotumia. Tuache tabia ya kuweka programu nyingi katika kompyuta zetu ambazo kwa hali ilivyo hatuzitumii kabisa. Kwa kawaida programu hujaza nafasi, kuweka uchafu na hatimaye kuiweka kompyuta matatani.

Kumbuka unapoweka (install) baadhi ya programu katika kompyuta yako, nazo huweka programu nyingine zinazoambatana nazo bila ya wewe kujua. Hatimaye unajikuta umelundika lundo la programu.
Tuangalie mfano huu; unapoweka programu ya Microsoft office, tafiti zinaonyesha watumiaji wengi hutumia programu kubwa tatu ambazo ni Word, Excel na Power Point.

Ieleweke kwenye kila bunda la programu ya Microsoft kuna programu nyingine zaidi ya kumi ndani yake ambazo zote huwekwa pamoja, lakini hazitumiwi kabisa au zinatumiwa mara chache mno.

Wataalamu wanashauri tunapotaka kuweka programu tuchague kile kwa kuzingatia kile kinachojulikana kama ‘custom Installation’. Uwekaji wa aina hii siyo tu unaweza kukuelekeza wapi uweke programu, bali pia utaweza kuchagua aina ya programu unazotaka kuweka kwenye kompyuta yako.

Pili, hakikisha unatumia programu zinazokwenda na wakati. Fanya uboreshaji wa matoleo mapya ya programu unazotumia (update)unapohitajika. Tuache hofu ya kutumia uboreshaji kwa hofu ya kufutiwa usajili wa programu au labda yataathiri kompyuta yako.

Cha muhimu kuzingatia ni kuwa kila yanapotoka matoleo mapya, wahusika wanalenga kutusaidia watumiaji na siyo vinginevyo.

Tumia programu halisi

Hakikisha unatumia programu halisi au kuichukua moja kwa moja kutoka kwenye wavuti ya watengenezaji au sehemu salama kama ilivyoelekezwa na mtengenezaji.

Kuwa na programu halisi sio tu itaiwezesha kompyuta yako kuwa imara, bali pia itakuwezesha kupata maboresho pindi yanapotoka kama tulivyoelezea hapo juu. Kiuhalisia, programu nyingi bandia (siyo zote) huvunja mfumo asili wa programu na kuifanya iwe dhahifu, huku nyingine zikipandikiza minyoo kwa mtindo wa viraka (patch) inayokwenda kuharibu mwendendo wa programu halisi.

Kwa mtindo huu unarahisisha kifaa chako kushambuliwa. Hivyo, matumizi ya programu bandia hasa kwa mitambo endeshi ni hatari kwa usalama wako.

Leo hii katika baadhi ya ofisi, wataalamu wa Tehama huweka mitambo endeshi bandia bila uongozi kufahamu, hivyo kuiweka kampuni kwenye hatari ya uvamizi.

Ushauri kwa wenye kampuni, wahakikishe wanatafuta Mkaguzi wa Tehama (IT Auditor) afanyie tathmini ya vifaa vyote ili kubaini dosari kama hizi.

Tumia programu za uhakika

No comments:

Post a Comment

PLEASE LEAVE YOUR COMMENTS HERE. HELP BLOG DEVELOPMENT

Print It: