Thursday, October 31, 2013

WA MITEGO NA SARE ZA POLISI



Dar es Salaam. Siku chache baada ya kukamatwa kwa tuhuma za kutumia sare za polisi bila kibali katika video ya wimbo ‘Salamu Zao’, na kisha kufikishwa katika Kituo cha Polisi Urafiki Manzese Jijini Dar es Salaam, rapa wa muziki wa kizazi kipya, Ney Wa Mitego amesimulia mkasa mzima na kusisitiza kuwa wabaya wake ndiyo waliycheza mchezo huo.

Akizungumza na Mwananchi, rapa huyo alisema sare hizo za polisi zilishonwa kwa ajili ya kazi hiyo na wala hazikuwa sare halisi za kipolisi.

“Mavazi haya ya kipolisi yalikuwa rasmi kwa ajili ya kutengeneza video ya Salamu Zao na hayakuwa halisi, ila nilishangaa pale nilipokamatwa na watu wasiojulikana jumamosi ya wiki iliyopita wakati tukitengeneza video, wakidai kwamba wao ni askari.Walinichukua hadi kituo cha urafiki, pale niliwekwa sero kwa kipindi cha dakika 20 hivi, baada ya kutoa maelezo ya kutosha niliachiwa”.

Baada ya kuachiwa, alirudi na kukamilisha kazi yake ambayo ameweka wazi kuwa itakuwa hewani wiki hii.

“Video ya Salamu Zao itaachiwa hewani Ijumaa ya wiki hii, hivyo watarajie kitu kipya na adimu kuonekana,” alisema Nay na kuongeza “Sijajua bado ni nani aliyenichomea lakini naahidi kuwa itaendelea kula kwao wale wote wanaonichukia na kamwe siwezi kuacha kuusema ukweli.”

Uongozi wa kituo cha Polisi Urafiki jijini Dar es Salaam ulithibitisha kumtia mbaroni msanii huyo kwa kukutwa akitumia sare zinazofanana na mavazi ya polisi kinyume cha sheria. Ofisi mmoja wa polisi ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini anasema waliamua kumuachia kwa vile waliridhika na maelezo yake.

No comments:

Post a Comment

PLEASE LEAVE YOUR COMMENTS HERE. HELP BLOG DEVELOPMENT

Print It: